April 7 2012 ni siku Steven Kanumba aliyofariki. Katika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake Watanzania kutoka sehemu mbalimbali watakutana Leaders Club kwa lengo la kumuenzi na kuangalia yale aliyofanya katika enzi za uhai wake pamoja na Uzindizi wa Filamu yake ya Mwisho.
Hii ni Filamu itakayoziduliwa na Jacklen Wolper katika Kumuenzi Steven Kanumba |
Kabla ya kifo chake Kanumba alikua amesaini mkataba ambao
ungemfanya awe staa mkubwa kuliko wote Afrika Mashriki. Meneja wake wakimataifa
Prince Richard ambaye ni mzaliwa wa Ghana alisema kuwa mkataba wake ungemfanya
Kanumba Aigize filamu tatu kubwa
Filam ya kwanza iIitwa Bleeding Sunshine na trail ilifanyika
Accra mwezi October mwaka jana. Filam hiyo ingefanyika Accra Misri na Dubai, Japo haikujulikana angeigiza uhusika gani angekua mtanzania wa kwanza Filam zaHollywood
na angeigiza na mastaa wakubwa wane wa marekani
Filamu hiyo ingezinduliwa Marekani, Canada,Uingereza, Afrika
Kusini,Ghana, Nigeria na hatimaye Tanzania
Katika Filamu ya Pili alikua Aigize Filamu ya Hollywood
iitwayo President’s First Love akishirikiana na Rose Ndauka Pamoja na Lusy Komba
Filamu hiyo kuhusu kiongozi wa Afrika Ingefanyika nchini Ghana kuanzia July na
August mwaka Jana
Filamu ya tatu ni Charity ambayo ingeanza kushutiwa April 14
nakumuhusisha pia muigizaji Lucy Komba. Tarehe ya kuigiza Filamu hiyo
ilingiliana na mwaliko aliokua ameupata kutoka kwa tamasha la Filamu la San
Fransisco Marekani, Huko alitakiwa kwenda kuzungumza uwezekano wa Bongo Movies
kuonyeshwa kwenye Tamasha la mwaka huu, 2013. Bahati mbaya kifo kilimwita
Haya ni baadhi ya matukio ya picha Yalio katika Filamu Yake Ya mwisho Itakayo Zinduliwa 7/4/2013 Leaders Club
No comments :
Post a Comment